KINGSBLOOD
de Kala
Nakiri nilikuumiza sana mama yangu
Nyumbani kukugonganisha na machangu
Pia kukugombanisha na ndugu zangu
Ili mradi nifurahi ndani ya nafsi yangu
Nakunywa ninalewa na rafiki zangu
Nakuangushia kipigo na una mimba yangu
Mpaka mimba ikachoroboka kwa ujinga wangu
Leo nitaficha wapi mimi sura yangu?
Mbele sioni kitu zaidi ya ukungu
Na maadui wako wengi zaidi ya nywele zangu
Nishike mkono mikosi inaniandama
Na usipo nionea huruma haki ya nani nitazama
Mwili hauna nguvu kama mwenye homa
Nahisi niko kuzimu na shetani ananichoma
Ongea chochote na nafsi yangu itapona
Nakiri sitorudia tena mbele ya Maulana
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Nisamehe nitakufa, kwa mawazo ya msongo
Wapambe walionipamba, wamenigeuzia mgongo
Baada ya kuishiwa pesa, wanadai sina mpango
Ni kweli sina dini, wala sina mchongo
Siku hizi sinywi bia, ni viroba mixer gongo
Nisikufiche, nimepoteza malengo
Kwenye kupa kwa mizigo, kwenye lori mi ndio tingo
Maisha yangu yanaelekea ukingo
Na kama nitakufa leo, jua kuu uliacha pengo
Nikiongea sana nikajitukana
Maana nilifungwa macho na starehe za ujana
Nikajiita pimpi kicheche bonge la bana
Nikakupa mateso ya moyo, mwili kimwana
Na kila nilipolewa ni kichapo cha kufana
Nishike mkono japo nimelewa sana
Sema neno moja liuponye mwili wenye laana
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Nakiri sina uti, ila sasa nakwangukia
Unanijua vizuri, sina haja ya kuhadithia
Ila sirudii makosa haki ya Mungu naapia
Sauti za kuzimu ninazisikia
Bila msamaha wako hakika nita disappear
Mi kipofu niongoze, natanga sioni njia
Nakiri mi ni bonge la fala tena mburula
Nilikuona taka-taka nikazurura
Nikapiga chaka kwa chaka na kina Shura
Sasa cheki nilivyo, nimenyooka kama rula
Natamani ardhi ipasuke nijifiche sura
Ama kweli dunia imenielemea
Mzigo ni mzito Golgotha naelekea
Ndugu wa damu yangu, sioni walikoelekea
Hakika ni wewe pekee unaweza kunitetea
Nadhani sasa sina tena cha kuongea
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Más canciones de Kala
-
The Wonder
Funktastic Groovers
-
Lucky Lu - Boogie Knight Remix
Straight Outta Space
-
Visage
Funktastic Groovers
-
Intro Tale
Tick Tack Tales
-
Flying Fish
Funktastic Groovers
-
Faraway Tree
Flow Festival 2018
-
Fantabulous (feat. Nils)
The NeverEnding Groove
-
Electric Joke
Believe in Forest
-
Midnight
Black Day Dream
-
Si Te Digo Que No
Si Te Digo Que No
-
TT
Tick Tack Tales
-
The Promise
Tick Tack Tales
-
Close Your Eyes
Tick Tack Tales
-
Not That Way
Tick Tack Tales
-
Tick Tack
Tick Tack Tales
-
Dream
Tick Tack Tales
-
Funk Meter
Tick Tack Tales
-
Tripple Gubbe
Tick Tack Tales
-
Broken Hearted
Broken Hearted
-
Flying Too Close To The Sun
Flying Too Close To The Sun