Paramount
de Jeremiah Bligen
Nakiri nilikuumiza sana mama yangu
Nyumbani kukugonganisha na machangu
Pia kukugombanisha na ndugu zangu
Ili mradi nifurahi ndani ya nafsi yangu
Nakunywa ninalewa na rafiki zangu
Nakuangushia kipigo na una mimba yangu
Mpaka mimba ikachoroboka kwa ujinga wangu
Leo nitaficha wapi mimi sura yangu?
Mbele sioni kitu zaidi ya ukungu
Na maadui wako wengi zaidi ya nywele zangu
Nishike mkono mikosi inaniandama
Na usipo nionea huruma haki ya nani nitazama
Mwili hauna nguvu kama mwenye homa
Nahisi niko kuzimu na shetani ananichoma
Ongea chochote na nafsi yangu itapona
Nakiri sitorudia tena mbele ya Maulana
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Nisamehe nitakufa, kwa mawazo ya msongo
Wapambe walionipamba, wamenigeuzia mgongo
Baada ya kuishiwa pesa, wanadai sina mpango
Ni kweli sina dini, wala sina mchongo
Siku hizi sinywi bia, ni viroba mixer gongo
Nisikufiche, nimepoteza malengo
Kwenye kupa kwa mizigo, kwenye lori mi ndio tingo
Maisha yangu yanaelekea ukingo
Na kama nitakufa leo, jua kuu uliacha pengo
Nikiongea sana nikajitukana
Maana nilifungwa macho na starehe za ujana
Nikajiita pimpi kicheche bonge la bana
Nikakupa mateso ya moyo, mwili kimwana
Na kila nilipolewa ni kichapo cha kufana
Nishike mkono japo nimelewa sana
Sema neno moja liuponye mwili wenye laana
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Nakiri sina uti, ila sasa nakwangukia
Unanijua vizuri, sina haja ya kuhadithia
Ila sirudii makosa haki ya Mungu naapia
Sauti za kuzimu ninazisikia
Bila msamaha wako hakika nita disappear
Mi kipofu niongoze, natanga sioni njia
Nakiri mi ni bonge la fala tena mburula
Nilikuona taka-taka nikazurura
Nikapiga chaka kwa chaka na kina Shura
Sasa cheki nilivyo, nimenyooka kama rula
Natamani ardhi ipasuke nijifiche sura
Ama kweli dunia imenielemea
Mzigo ni mzito Golgotha naelekea
Ndugu wa damu yangu, sioni walikoelekea
Hakika ni wewe pekee unaweza kunitetea
Nadhani sasa sina tena cha kuongea
Najua unanisikiaaa
Ila kunijibu ndo huwezi
Eeeh Mungu baba saidiaaa
Umlaze mahala pema mpenzi
Na pia anisamehe maha, anisamehe
Na pia anisamehe sana, anisamehe
Más canciones de Jeremiah Bligen
-
Flying Fallen Skies
When Ravens Cry
-
Throne - Remix (Bonus Track)
The Flames Will Not Consume You
-
Still
When Ravens Cry
-
Forever
The Flames Will Not Consume You
-
Sunset
The Flames Will Not Consume You
-
GBA
The Flames Will Not Consume You
-
NFN
Fighting Stance
-
Allways
The Flames Will Not Consume You
-
Nobody
The Flames Will Not Consume You
-
Rich Young Ruler
Fighting Stance
-
I Will Not Stop
The Flames Will Not Consume You
-
Interpret a Dream
The Flames Will Not Consume You
-
Essential
The Flames Will Not Consume You
-
Pardon the Interruption
When Ravens Cry
-
Take a Drive, To
When Ravens Cry
-
Bleed
When Ravens Cry
-
Closer
When Ravens Cry
-
Waiting Room
When Ravens Cry
-
While They're Red
When Ravens Cry
-
Neverending...
When Ravens Cry