EATER

de HAWA

Kipya usichojua
Maana isielewe ka barani
Labda ulipogundua
Ukanunua kisu cha butchery

We ukanirarua
Leo kwako sina dhamani tena
Ibada niombe dua
Labda atarudi kuwa ka zamani

Ooh, ooh

Macho yangu yamekaa kusubiri
Kwa sababu ya kukesha
Na nikikesha kuna mawili
Huja usije kabisa

Moyoni naona dalili
Pendo nalichekecha
Tamu imegeuka shubiri
Mapenzi yamekwisha kabisa ee

Hata mi nina moyo, nina moyo
Usisahau nina moyo nina moyo
Ukumbuke moyo nina moyo
Wenye nyama moyo nina moyo

Hata mi nina moyo, nina moyo
Usisahau nina moyo nina moyo
Ukumbuke moyo nina moyo
Wenye nyama moyo nina moyo

Nina imani unavyoniliza leo
Na mi kesho Mungu atanilipia
Siamini mi nimegeuka kero
Sina chochote cha kukupa hisia

Hivi ni kweli ninayo yaona leo
Au niko ndotoni?
Mapenzi yamekuwa kwa leo
Yananichimbiwa shimoni

Macho yalalamika kusubiri
Kwa sababu ya kukesha
Na nikikesha kuna mawili
Huja usije kabisa

Moyoni naona dalili
Pendo nalichekecha
Tamu imegeuka shubiri
Mapenzi yamekwisha kabisa ee

Hata mi nina moyo, nina moyo
Usisahau nina moyo nina moyo
Ukumbuke moyo nina moyo
Wenye nyama moyo nina moyo

Hata mi nina moyo, nina moyo
Usisahau nina moyo nina moyo
Ukumbuke moyo nina moyo
Wenye nyama moyo nina moyo

(Nina moyo mama, nina moyo mama)

Más canciones de HAWA